Sunday, 22 October 2017

Matumizi ya Kadi za Benki katika Manunuzi Kwenye Mtandao

matumizi-ya-kadi-za-benki
Teknolojia inayowezesha matumizi ya kadi za benki kununua bidhaa katika maduka na mtandao wa kompyuta ni kitu kilichozoeleka na kufanyika sana katika nchi zilizoendelea hasa Ulaya na Marekani.
Lakini kwa Afrika ikiwemo Tanzania si jambo la kawaida sana. Japo kuna watu wachace ambao wanatumia.
Kuna fursa nyingi katika utumiaji wa kadi za benki kufanya manunuzi ya bidhaa na huduma,ikiwemo kununua bidhaa toka nje kwa bei nafuu ukilinganisha na kununua kwa wachuuzi wa maduka.
Bidhaa hasa za kielektroniki kama vitabu na programu za kompyuta au simu zinapatikana kwa urahisi kutoka katika masoko kupitia mtandao wa kompyuta.
Biadhaa nyingine ni zile halisi kama kamera,simu,komputa,vitabu na vingine vingi kutaja vichache vinaweza vikanunuliwa toka maduka ya nje ya nchi kwa bei nafuu na vyenye ubora mkubwa.

Kadi za Benki ni nini?

Hizi ni kadi za kuchukulia fedha katika mashine ya kutoa fedha(ATM) ambazo zinakuwezesha pia kununua bidhaa na huduma katika sehemu za mauzo kama mahotelini,maduka ya bidhaa(“Supermarkets”) na katika masoko ya kwenye matandao wa intaneti.
Kadi hizi zimeunganishwa na akaunti yako ya benki na kila unaponunua kupitia kadi hii kiasi cha fedha kinapunguzwa katika akaunti yako sawa na ghramaya bidhaa iliyonunuliwa.
Makampuni ya Benki yanafanya kazi na makampuni ya kimataifa ambayo yanawezesha mfumo huu wa manunuzi kufanya kazi kokote duniani. Baadhi ya makampuni makubwa duniani ni MasterCard na VISA
matumizi-ya-kadi-za-benki_mastercard
Kadi ya MasterCard
matumizi-ya-kadi-za-benki_visa
Kadi ya VISA
 Aina za Kadi:
Kuna aina mbili za kadi za manunuzi
i. Kadi za Malipo ya Mkopo-Creditcard:
Kadi hizi zinaruhusu mteja kununua hata kama hana fedha za kutosha katika akaunti yake na atarudisha mkopo baada ya muda ambao atapangiwa au fedha nyingine inapokuwa imeingia kwenye akaunti hiyo.
Aina hii ya kadi zinatumika zaidi katika nchi zilizoendelea,na aghalabu hutolewa na benki nchini Tanzania.
ii. Kadi za Malipo ya Awali-Debitcard:
Kadi hizi zinamuwezesha mteja kununua kama tu kuna fedha za kutosha katika akaunti yake vinginevyo manunuzi hayatawezekana.
Aina hii ya kadi ndizo ambazo zinatolewa kwa wingi nchini Tanzania.

Matumizi ya kadi za Benki katika Manunuzi:

Nchini Tanzania kwa sasa karibu kadi zote za benki zimeunganishwa na huduma hii na inawawezesha wateja wake wote wenye Kadi za MasterCard au VISA kuweza kununua katika mtandao na katika mashine zilizopo katika maduka na sehemu za huduma mbalimbali kama mahotelini. Pia kadi hizi zinawezesha wateja kutoa fedha katika mashine za fedha (ATM) zozote duniani na kuwawezesha wasafiri kutembea bila fedha wanapokuwa ndani na nje ya nchi.
matumizi-ya-kadi-za-benki_pos-1
Matumizi ya kadi za benki inatoa fursa kwa wafanyabiashara mbalimbali nchini Tanzania na nchi nyingine za Africa kuunganisha machine za malipo ambazo zinaweza kusoma kadi za benki na kurahisisha namna biashara zinanyofanyika.
Huduma za manunuzi ya umeme,mafuta katika vituo vya kuuza mafuta,maduka na hata ulipaji wa kodi mbalimbali. Utumiaji wa mfumo huu katika sehemu za huduma itasaidia kupunguza msongamano wa watu katika sehemu hizi za utoaji huduma kwa jamii.
Pia matumizi ya mfumo huu yatasaidia kupunguza hatari ya kutembea na fedha nyingi na kuvutia wezi barabani na nyumbani.

Faida za Matumizi ya Kadi za Benki Katika Manunuzi

i. Urahisi wa Kupata Huduma
Kutumia kadi kunarahisisha kupata huduma mahala popote, wakati wowote.
Hakuna sababu ya kwenda benki na kusimama katika mstari mrefu.
ii. Unafuu wa Bei
Kwa baadhi ya bidhaa hasa toka nje ya nchi zinaweza kupatikana kwa bei nafuu zaidi kuliko ukinunua toka dukani nchini kwako. Mfano ukinunua kitabu toka Amazon utapata kwa bei nafuu kuliko kununua katika duka la vitabu nchini Tanzania. Hii ni kutokana na gharama za kodi na usambazaji za wauzaji.
 iii. Kupunguza Wizi wa Fedha Taslimu
Ukitumia kadi kwa manunuzi huhitaji kutembea na fedha nyingi mfukoni hivyo kupunguza hatari ya kupoteza au kuibiwa.
iv. Usumbufu wa Kutembea na Fedha Taslimu
Matumizi ya kadi yanaondoa usumbufu wa kutembea na fedha nyingi mfukoni au kutunza majumbani.

 Na Hasara Je?

Kama ilivyo kwa vitu vingine vingi vizuri pia havikosi ubaya kwa upande wa pili:
i. Hatari ya Wizi wa Mtandao
Kumekuwa na matukio ya wizi wa fedha kupitia mtandao na kutumia kadi yako kwa manunuzi kwa jinsi isiyo salama inaongeza hatari ya kuibiwa na wezi katika mtandao.
Hili linaweza kudhubitiwa kwa kuhakikisha unafuata sawa sawa masharti ya usalama kama vile kutogawa namba ya siri kwa yeyote na kutunza kadi sehemu iliyo salama.
 ii. Utegemezi Katika Uwepo wa Mtandao
Kwakuwa kazi zinatumia mtandao kunafanya ukose huduma kama mtandao unakuwa umekatika. Hii inaweza ikakuchelewesha kupata huduma stahiki kwa wakati.
 iii. Kutumia Fedha Kupita Kiasi
Matumizi ya kadi katika manunuzi yanaweza yakakushawishi kutumia zaidi kuliko kama ungetumia fedha taslimu. Hivyo ni muhimu kukuwa na bajeti na kuifuta.
iv. Gharama za Ziada
Kuna gharama za kufanya mwamala katika mtandao ambazo wakati mwingine zinaweza zikafanya bei kuwa kubwa kidogo kuliko kama ungetumia fedha taslimu.

Muda wa Kuhama Umefika?

Bila shaka wakati umefika sasa kwa waafrika kuhamia katika teknolojia hii ya benki,kuna idadi kubwa tayari wanatumia kadi hizi nikiwemo mimi mwenyewe na inaleta mapinduzi makubwa sana kwenye urahisi wa manunuzi na matumizi mazuri ya muda.
Matumizi ya kadi za benki katika mfumo wa manunuzi na malipo itaboresha sekta ya biashara na hata kwa wakulima wa vijijini ambako mtandao wa intaneti umefika au unaweza kufika wataweza kufaidika nayo pia.
Afrika na mataifa yake inapaswa kufahamu kuwa matumizi ya teknolojia kwa njia iliyo sahihi inasaidia sana maendeleo ya nchi kama ambavyo imetokea katika nchi zilizoendelea.
Kama serikali ikitengeneza mfumo mzuri katika taasisi zake kama TRA,Wizara ya fedha,TANESCO na mashirika mengine ya huduma na udhibiti wa fedha ikiwemo benki kuu mfumo huu unaweza ukatumika katika biashara nchini na kuongeza tija na ufanisi.

USHAA IONA HII SASA WAWEZA KUTUMIA SIMU YAKO YA MKONONI KAMA REMORT CONTROL YA TV AU VIFAA VINGINE

KALI%2Bcopy
New Trick
Habari za wakati huu msomaji wa Blog yako pendwa ya DODY BLOG ! Katika mfululizo wa makala za wiki hii, leo tutaangalia jinsi ya KUTUMIA  simu yako hio ya SmartPhonekama Mouse ya kompyuta.

FAIDA
>>>Hii inaweza kukusaidia pale ambapo hauna Mouse kwa ajili ya compyuta yako, au TouchPad ya Laptop yako haifanyi kazi! Yani inasumbua!

MAHITAJI
>>Utahitajika kuinstall program na App ntakazokupa hapa chini! Unaweza kutumia Apps mbalimbali na step ni hizihizi. Host file utaiinstall kwenye kompyuta yako na App utaiweka kwenye simu yako, halafu utaunga compyuta yako kwenye wireless ya simu yako au bluetooth! (Lengo la kuunga ni kuweka mawasiliano kati ya simu na kompyuta). kwa hio unaweza kutumia Bluetooth au Wireless! Zote ni sawa ila hapa nitaelezeaWireless.

HATUA KWA HATUA

1.  Download na install Monect kwenye simu yako HAPA!

2
Install Monect Portable


2. Kwenye PC yako download na install Monect Host kwa kuclik HAPA! File lina MB 28 tuu, kwa hio usiwasingizie Voda. Download na extract vilivyopo kwenye hio Zip File, na chagua lililoandikwaMonectHost, na uliinstall.


3
Download Host


KUMBUKA; Wakati unadownload hio host file, pc yako inaweza kukwambia kwamba hilo file ni Malicious,weka chagua keep file, ili kuweza kuendelea na step za mbele. See picture here>

4
Chagua Keep

>Na pia windows firewall inaweza ikakupa alert, we chagua Allow Access.

5
Allow Access

3. 
Hakikisha simu na kompyuta yako umeviunganisha kwa Wi-fi. Kwenye simu nenda Setting>>>Mobile Networks>>>Tethering and Portable Hotspot, weka settings hapo then iweke ON, na uiunge kwenye PC yako.

4. Tufanye sasa kompyuta na simu yako zipo kwenye Wireless moja, na hio MonectHost umeifungua kwenye kompyuta yako, ifungue ile Monect App ya simu na chagua/click Search Host,ikitokea IP adressya PC yako Connect. Kama unaijua IP ya compyuta yako, unaweza kuiingiza moja kwa moja. Kama inakataa ku connect, jaribu ku restart kompyuta yako na uhakikishe MonectHost umei install vizuri.

6
IP itaonekana ya PC yako

5. Ikishakuwa connected utaona options mbalimbali 12. Kila moja ina kazi yake, leo tutatumia Touch Pad,sababu ndio lengo la makala hii. Tazama picha hapa chini.

7
Options mbalimbali

6. Touch Pad inaifanya simu yako kuwa kama ile Mouse ya Laptop (TouchPad) na inakuwa sehemu ya kutembeza vidole, ku right click, ku scroll ,a ku select kama mouse ya kawaida. Kwa hio ifanyie mazoezi na utakuwa na uwezo wa kuitumia kwa umbali wowote ambapo Wireless itakuwa bado ipo connected.

8


7. Pia kuna options mbalimbali ambazo unaweza pia kuzitumia hapo.

9
Jifunze kuzitumia zote hizi

Kumbuka utaalamu huu umeletwa kwenu kwa ushirikiano wa Technology Homesite na Slaus Technologies Tz1 Team, na kama una swali usisite kutuandikia hapo chini kwenye comments, au wasiliana nasi kwaa njia hizi HAPA!

SOMA MAKALA NYINGINE KAMA HIZI HAPA!

WEKA MATANGAZO YA SEEBAIT KWENYE BLOG YAKO NA ULIPWE

[​IMG]
Habari ndugu zangu katika tech leo tutazungumzia kuhusu kujiinua kiuchumi sisi kama blogger's, nalizungumzia hili baada ya kupata maswali na maoni kuhusu seebait kutoka kwa blogger's wenzangu hivyo tunatimiza Ahadi kama kawaida yetu, naam nisikupotezee wakati twende kwenye mada moja kwa moja.

Jinsi ya kujiunga na seebait hatua kwa hatua hatua ya kwanza ingia kwenye site ya Seebait.com kisha bonyeza sehemu iliyoandikwa Login/SignUp 
[​IMG]
Itaonekana muonekano kama huu pichani
Itakuletea muonekano huo pichani , kwasababu sisi ndio tunahitaji kujipatia pesa kupitia Seebait.com basi tutaenda sehemu iliyoandikwa Select option you want to use kisha chagua mtandao unaohitaji kujisajili seebait kupitia mtandao ulioidhinishwa na seebai ambao ni Facebook, twitter na google+ hivyo nitakuonyesha kupitia google+ kwasababu bloggers wengi tunatumia google+
[​IMG]
ukibonyeza google+ itakuomba idhini hivyo bonyeza Allow, 
[​IMG]
Itakuwezesha kuingia katika dashibodi ya seebait kama inavyoonekana pichani kisha utucopy hizo code na kwenda kuzipaste kwenye blog yako
[​IMG]
Katika dashidadi ya seebait walishakuelekeza sehemu ya kuweka , hivyo ingia kwenye blog yako bonyeza theme kisha edit Html, kisha search maneno haya <head> [ jinsi ya kutafuta code kwenye HTML bonyeza mouse yako mara moja kwenye code za templete yako kisha bonyeza Ctrl+F utaona sehemu ya kusearch] kisha paste code za seebait chini ya code hii <head>. save tempalte yako.
kisha rudi kwenye website ya seebait.com bonyeza sehemu inayosomeka Properties , kisha bonyeza Add Property 
[​IMG]

Utaona fomu kama hiyo hapo juu pichani jaza fomu hiyo kama hapa chini pichani
[​IMG]
Hiyo picha hapo juu ni mfano hivyo jaza kutokana na mahitaji ya blog yako hakikisha hauvunji sheria zaseebait.com, kisha ukimaliza bonyeza Submit
[​IMG]
Ukisha submit itakuletea muonekano huo hapo juu kama umekidhi mahitaji ya seebait , lakini kuna vitu vitapungua kutokana na picha yangu ipo aproved lakini yako haitakuwa aproved kwasababu bado hajakubaliwa na kwenye status itakuonyesha not verify hivyo tumalizie hivi bonyeza sehemu yenye alama ya mshale ulioelekea chini unapatinaka upande wa kulia wa properties yako , utaidownload properties yako kupitia mshale huo, kisha ifungue kwa ku doble-click , itafunguka kupitia browser yako mimi nimetumia Chrome pichani hapa chini
[​IMG]
Utaona code mfano wa hizo hapo juu sasa andaa code zako kwaajili ya ku verify akaunti yako ya seebait , pia seebait wameelekeza kuhusu kukamilisha hilo nenda juu kabisa kulia kwenye dashibodi ya seebait utaona alama ya magazine bonyeza hapo kisha tafuta Property Activation 
[​IMG]
Utaona makala hiyo ya msaada wako imekuwa nambari moja bonyeza neno Read itafunguka makala kisha copy code hii <meta name="seebait" content="ACTIVATION CODE HERE" /> Kisha paste sehemu unayodhani utaweza kuiedit mimi huwa natumia notepad kisha irekebishe hapo kwenye neno ACTIVATION CODE HERE paste zile code za kwenye file ulilodownload kwenye properties hivyo code zako zitakuwa hivi <meta name="seebait" content="ryyady-bhay49d26e96ac7ebfc7c9t.html" /> Chukua code zako hizo ulizozitengeneza vema kisha nenda kapaste chini ya kwenye code hii <head> hii tulishazungumzia sehemu ya kuipata kwenye maelezo yetu hapo juu.

kisha rudi tena kwenye dashibodi ya seebait.com nenda kwenye properties kulia bonyeza alama ya TIKI au Nike utaona mabadiliko sehemu ya status itaandika Active. 
kufikia hapo umefanikiwa kuwa na akaunti ya seebait malizia kuweka matangazo kisha subiri seebait.comwaipitie fomu yako ya maombi kama umekamilisha utakuta notification kwenye dashibodi yako yaseebait.com
[​IMG]
Mpaka hapo utakuwa umefanikiwa sasa jitahidi kutafuta Traffic kwa nguvu ili upate pesa zaidi
All the best