Saturday 28 September 2019

wamiliki wa magroup ya watsapp kenya kuwa na leseni

Katika kudhibiti majukwaa ya mitandao ya kijamii, watawala nchini kenya wamependekeza muswada ambao utawalazimisha watu walioanzisha makundi ya WhatsApp, Facebook na Wanablogi kuwa na leseni kutoka mamlaka ya mawasiliano ya Kenya.

Muswada huo ambao tayari umeshapelekwa Bungeni unataka Viongozi (Administrators) wa makundi ya WhatsApp kuwa na leseni na kuwasajili wanachama (Members) wa kundi na pia kujua anuani zao za mahala wanapoishi.

facebook whatsapp apps leseni za whatsapp

Na pia kuweka wazi kile kinachojadiliwa ndani ya kundi kwa jeshi la polisi. Kiongozi wa kundi atalazimika kujaza majina ya wanachama wake pamoja na anuani zao wakati wa kujaza fomu maalumu ya kupata leseni ya uendeshaji wa kundi lake.
Pia Viongozi hao watatakiwa wawe na wanachama waliofikia miaka 18 au zaidi.
Endapo muswada huo utapita basi yeyote atakayeendesha Kundi bila ya Leseni atakumbana na adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja Gerezani au faini ya Kshs 200,000/- (Takribani Tshs 400,000/- )

No comments:

Post a Comment